VIDEO: Ufafanuzi alioutoa mbunge aliyedaiwa kupokea mishahara hewa ya miezi mitano


Gazeti moja la kila siku, jana liripoti likidai kuwa Mbunge wa Makete ‘CCM’, Prof. Norman Sigalla ambaye alikuwa mkuu wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma amekuwa akipokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa miezi mitano wakati alikwisha acha kazi hiyo alipoteuliwa kugombea ubunge wa Makete na kushinda.

Ilidaiwa kuwa hata baada ya kuacha kazi hiyo ya ukuu wa wilaya aliendelea kupokea mshahara wake wa ukuu wa wilaya wa milioni 4.6 kutokana na ofisa utumishi wa ofisi ya katibu tawala mkoa wa Ruvuma kumrudisha kwenye orodha ya malipo ya mshahara.

Leo kupitia kipindi cha clouds 360 cha Clouds TV, Prof Sigalla ametoa ufafanuzi wa tuhuma hizo ambapo amekanusha na kusema kiasi cha fedha kilichoingia kwenye akaunti yake kwamba si sh milionI 23 bali ni sh milioni 5 ambazo zilikuwa hazieleweki.

Hata hivyo amesisitiza kuwa baada ya kugundua kuwa pesa imeingizwa kwenye akaunti yake kabla hata ya gazeti kuripoti alimwandikia katibu wa bunge kumtaka kuanzia August akate fedha hizo kwenye mshahara wake, kuzirudisha hazina kuu na RAS achukuliwe hatua kwa kuingiza fedha kwenye akaunti isiyotumika.

0 comments:

Post a Comment