VIDEO: Maneno ya Profesa Anna Tibaijuka kwa wanaosema alizikataa mil 200

Siku chache baada ya Waziri wa zamani wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka kushinda tuzo ya kimataifa ya “His Royal Highness Prince Khalifa bin Salman Al Khalifa Award for Sustainable Development” nchini Marekani na kuzikataa fedha zaidi ya milion 200 alizotakiwa kupewa kwa hofu ya kuhusishwa na zile tuhuma za Escrow
Kilichotokea kwenye hii tuzo wanayosema nimekataa haina tofauti na pesa za Rugemalila, sikukataa fedha hizo zaidi ya mil 200 bali sikuweza kuzichukua kwasababu ya kisheria kwakuwa yangenikuta yaleyale ya Escrow‘ –Prof Anna Tibaijuka
Mimi mwenyewe nimeziacha fedha hizo kwa masikitiko makubwa kwakuwa sheria imenifunga, Sheria ya maadili ya nchi inasema kiongozi haruhusiwi kuchukua zaidi ya elfu hamsini sasa ningezichukua kwangu ingekuwa kizungumkuti‘ –Prof Anna Tibaijuka
Kwahiyo mimi nikawaambia kule kwetu sheria ni ngumu kwahiyo nikawaambia hizi fedha naziacha mezani kisha tukajipange na pia kama mnaweza itabidi hizi fedha ziende zikawasaidie wananchi wa Tanzania kwenye matatizo yao‘ –Prof Anna Tibaijuka
Unaweza kuendelea kumsikiliza Profesa Tibaijuka kwenye hii video hapa chini…

0 comments:

Post a Comment