Monastar amtole povu Shilole, kisa kipo hapa

Monastar

Monastar ni mmoja wa wasanii waliokuwa chini ya kile alichokiita bendi ya shilole ambapo walikuwa wasanii 3.Monastar,Gaucho na Amadai.

Kilichotokea ni kuwa mambo yameenda kinyume na makubaliano yao.Kwa mujibu wa Mona walikubaliana na shilole kuwa atakuwa akienda nao kwenye show zake zote na kabla hajapanda jukwaani angewatanguliza wao jambo ambalo amelifanya mara kadhaa kwenye show za Dar es salaam.
 
Shilole

Mona ameiambia planetbongo kuwa ghafla mambo yalianza kubadilika na Shishi akaanza kumpendelea zaidi mmoja wao ambaye ni Amadai.

Huyu amadai ndiye yule ambaye kulikuwa na tetesi anatoka kimapenzi na Shilole.Hata hvyo mona alikataa kuzungumzia issue ya mahusiano ya wawili hao akisema ni mambo yao private ila ambacho hajaridhishwa nacho ni shilole kwenda kufanya show mikoani akiwa na amadai peke yake.

Amesema wamefanya kazi muda mrefu na Makubaliano yao yalikuwa waondoke wote watatu kwenye mikoa yote alipopata show lakini dakika za mwisho wakashtukia amesepa na amadai.

Shilole bado hajapatikana kujibu shutuma hizi.

– Leproducer

0 comments:

Post a Comment