Feza Kessy Anahisi Nando Anadata ‘Atafutwe na Asaidiwe’

Staa aliyewahi kuiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, Feza Kessy, amesema kuwa anaamini Nando aliyewahi kushiriki naye kwenye shindano hilo, amepatwa na tatizo au anaugua kwakuwa tabia anazozionyesha zinampa mashaka.

Akiongea kwenye kipindi cha Kubamba kupitia Times FM, Feza amesema anaona akili ya Nando kama imevurugika kwa sasa. Anasema amekuwa tofauti na Nando, yule kijana mwenye nidhamu na mpole aliyekuwa akimfahamu.

“Naamini Nando ana tatizo asaidiwe,” alisema Feza. “Sijui kwanini lakini naamini Nando ana something hayupo sawa, sio yule Nando ninayemfahamu, naomba atafutwe asaidiwe,” alisisitiza.

Feza ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa Choice FM, amedai kuwa aliwahi kukutana na Nando na akampa noti ya shilingi elfu 10. Anasema badala yake yake staa huyo aliitupa chini kwa madai kuwa haiwezi kumsaidia kitu.

0 comments:

Post a Comment