VIDEO: Babu Tale ameongelea ukaribu wa Diamond Platnumz na Ommy Dimpoz

Najua kama utakuwa mfuatiliaji wa mastaa wa bongoflevani utafahamu ukaribu aliyokuwa nao Diamond Platnumz na Ommy Dimpoz hapo awali ambapo pia walishafanyaga collabo ya pamoja na mwanadada kutoka Kenya, Victoria Kimani ya ‘Prokoto‘ na walikuwa wakionekana mda mwingi wapo pamoja hata kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram wakipost picha wako pamoja.

Lakini kwa sasahivi imekuwa kimya na inaonekana kila mtu anafanya issue zake na hii imeleta utata kwa mashabiki kuhisi kuwa labda kuna beef kati yao ama vipi, Camera za Millardayo.com na AyoTV zimeweza kumpata mananger wa Diamond Platnumz, Babu Tale na haya ndio yalikuwa majibu yake…

>>>’Sijawah kuwaona hivi karibuni labda kwasababu kila mtu mmoja anapiga issue zake lakini me na Ommy tulisafiri wote na Naseeb mpaka uingereza na tukafanya video ya BamBam sijawahi…’

0 comments:

Post a Comment