DEREVA Bodaboda Aliyembeba Mmiliki wa Nyoka wa Ajabu Afunguka A-Z (Video)

Tukio lililozua taharuki kwa wakazi wa Songea mkoani Ruvuma na kupewa nafasi kubwa katika vyombo vya habari vya Tanzania na nje ya Tanzania pamoja na mitandao ya kijamii, huku likiacha gumzo midomoni mwa watu, kuhusiana na kifo cha Denis Komba kufariki dunia baada ya nyoka wake aliyekuwa anasadikiwa kummiliki, kuuawa na wananchi DESEMBA 26.

Ruvuma TV imezungumza na KASIANI HAULE, ambaye ndiye dereva boda boda aliyekuwa kakodiwa na marehemu DENISI KOMBA Bonyeza hiyo Video upate ukweli wa tukio.

MAKUBWA Yafichuka Faru John

Maofi sa wa Wizara ya Maliasili na Utalii, wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) na maofi sa Taasisi ya Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) wakiwamo madaktari, wakifanya uchunguzi wa Faru John baada ya kufa katika eneo la Sasakwa Grumeti.


SAKATA la kutoweka kwa faru John lililoibuliwa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika mikoa ya Arusha na Manyara linazidi kuchukua sura mpya kila kukicha.

Taarifa zilizolifikia MTANZANIA baada ya kufanya uchunguzi wa sakata hilo kwa wiki kadhaa sasa, zinaonyesha kwamba uamuzi wa kumhamisha faru huyo kutoka Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro ulihusisha mamlaka za kitaifa za Serikali.

Habari kutoka vyanzo vya kuaminika zinaeleza kwamba mchakato wa kuhamishwa kwa faru John kutoka Hifadhi ya Bonde la Ngorongoro kwenda Grumeti, ulianza katika eneo la Nyasirori ndani ya Hifadhi ya Serengeti Aprili 17, 2015.

Uamuzi huo kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika serikalini, ulianza siku hiyo hiyo wakati wa tukio la kuwafungulia mbwa mwitu waliokuwa wamehifadhiwa katika eneo maalumu huko Nyasirori.

Vyanzo vya uhakika vya habari vinaeleza kwamba mjadala kuhusu kuhamishwa kwa faru John ulifanyika wakati watendaji wakuu wa taasisi za uhifadhi za Serikali zinazounda Kamati Maalumu ya Kuwalinda Tembo na Faru (National Elephant and Rhino Steering Committee) wakiwapo.

Miongoni mwa watendaji wanaotajwa kuwapo wakati wa mjadala kuhusu kuhamishwa kwa faru huyo kutoka katika Bonde la Ngorongoro kutokana na sababu za kitaalamu, ni Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro (NCAA), Dk. Fadhili Manongi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Allan Kijazi.

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti ya Wanyamapori (TAWIRI), Dk. Simon Mduma na mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori aliyefahamika kwa jina la Alex Choya.

Taarifa kuhusu kuwapo kwa haja ya kuhamishwa kwa faru huyo zilipelekwa hadi Wizara ya Maliasili na Utalii.

Kufikishwa kwa suala hilo wizarani kulifuatiwa na hatua ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk. Adelhem Meru, kuwaandikia barua watendaji wa Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro kutekeleza uamuzi huo ifikapo Desemba 31, 2015.

Alipoulizwa kuhusu uwapo wa barua hiyo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, alisema ni kweli barua hiyo ipo kwenye kumbukumbu za wizara.

“Ni kweli hiyo document ipo, lakini hili suala la faru John linafanyiwa kazi na vyombo vya dola. Nadhani si vizuri kulijadili kwa undani sasa, tusubiri matokeo ya uchunguzi,” alisema Waziri Maghembe.

Wahifadhi kadhaa waliozungumza na gazeti hili kutoka Serengeti na Ngorongoro juu ya sakata hilo, walieleza kwamba kiini cha kufikiwa kwa uamuzi huo kulitokana na mabadiliko makubwa ya kitabia aliyokuwa nayo faru John tangu mwaka 2002.

“Faru John alizaliwa ndani ya Ngorongoro, na alianza kuonyesha tabia za ukorofi dhidi ya faru wengine madume mwaka 2002,” alieleza mhifadhi mmoja anayefanya kazi Ngorongoro.

Mhifadhi mwingine alimweleza mwandishi wetu kwamba hali hiyo ilisababisha Mamlaka ya Bonde la Ngorongoro kufanya mawasiliano na TAWIRI kuhusu hatua za kuchukua.

Alisema kuwa hali ilizidi kuwa mbaya na mwaka 2005 kiliitishwa kikao kingine kujadili matatizo ya faru John ambaye tabia yake ya kuwapiga faru wengine ilisababisha wanyama hao kutoka ndani ya Ngorongoro na hivyo kusababisha ugumu wa kuwalinda.

“Tatizo jingine lililotokana na ubabe wa faru John, ni gharama kubwa za ulinzi wa faru waliokimbia vipigo, na kutawanyika hadi kwenye mashamba ya watu.

“Faru wana tabia moja, pindi wanapopigana, yule aliyeshindwa huondoka eneo husika,” alieleza mhifadhi mwingine aliyezungumza na MTANZANIA.

Taarifa kutoka Ngorongoro zinaeleza kuwa mwaka 2013 tatizo la faru John lilizidi kuwa baya zaidi pale kreta, baada ya faru huyo kuua wenzake wawili.

Katika tukio hilo, faru John anatajwa aliua ndama (jike) kwa kumchoma na pembe na kisha akaua dume mwenzake katika mapigano.

Mhifadhi huyo aliliambia gazeti hili kwamba faru John ndiye aliyekuwa na watoto wengi katika Bonde la Ngorongoro kuliko faru mwingine yeyote.

Tukio la faru John kumuua ndama kwa pembe lilitokea wakati alipokuwa akijaribu kumpanda mama yake.

“Faru John alianza kuwapanda watoto wake, jambo ambalo kitaalamu si salama kwa uhai wa faru, hivyo kuendelea kumwacha pale kreta lilikuwa jambo la hatari.

“Baada ya matukio hayo ya 2013, kikao kilikaa tena ambapo TANAPA pia walihudhuria, swali kubwa likiwa ni wapi ambako faru John alipaswa kupelekwa?” alisema mhifadhi mwingine.

Kwa mhifadhi huyo, uamuzi wa kwanza ulikuwa ni kumtoa faru John na kumpeleka katika Hifadhi ya Mkomazi ambako kuna makazi maalumu ya faru (rhino sanctuary).

Hifadhi ya Mkomazi ambako hata hivyo uamuzi huo ulikwama, iko chini ya uendeshaji wa mwekezaji Tony Fitz John.

Kukwama kwa uamuzi huo wa kwanza pia kunaelezwa kulisababishwa na taarifa kwamba katika Hifadhi ya Mkomazi kulikuwa na uwiano sawa kati ya faru madume na majike.

Taarifa nyingine zinasema mwaka huo huo wa 2013, ulifikiwa uamuzi mwingine wa kumkata pembe faru huyo kama njia ya kupunguza madhara aliyokuwa akisababisha katika hifadhi, jambo ambalo lilifanyika.

Wakati wahifadhi wakiumiza vichwa kuhusu nini kifanyike, faru wawili waliokuwa Grumeti, waitwao Limpopo (dume) na Laikipya (jike) walipoteza maisha.

Taarifa zinasema Limpopo aliuawa wakati akipigana na tembo, wakati sababu za kifo cha Laikipya hazikutajwa.

Upungufu huo wa faru wawili ndiyo sababu ambayo baadaye ilisababisha kuzaliwa kwa hoja ya faru John kupelekwa Grumeti kupanda na kuzalisha majike.

Hali hiyo inatajwa kuwa ndiyo iliyosababisha uongozi wa Grumeti inayomilikiwa na tajiri wa Marekani, Paul Tudo Jones, waandike barua ya kuomba faru dume kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori, jambo ambalo lilifanyika.

Vyanzo vya habari kutoka serikalini vinaeleza kuwa baada ya maombi hayo, kilikaa kikao cha Kamati ya Tembo na Faru mjini Dodoma ambacho kilitoa mapendekezo yake kuwa faru John anafaa kwenda Grumeti.

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa ni pamoja na usalama wake, gharama kubwa za kumhamisha na suala zima la siasa kuhusu hatua hiyo.

Kwa hiyo taratibu zikaanza, ikiwamo kutafuta madaktari watakaoshiriki kumkamata, ambao miongoni mwao walikuwa kutoka Kenya.

Hatua ya kwanza ya kumhamisha kwa mujibu wa taarifa za wataalamu wa uhifadhi, ilikuwa ni kujengwa kwa banda maalumu ambalo faru John aliingizwa Novemba 7, 2015.

“Unajua kuna taratibu za kuhamisha faru, hamuwezi kumdunga sindano ya usingizi na kumbeba, unaweza kumjeruhi na hata kusababisha kifo, kwa hiyo tulimuacha azoee lile banda kwanza kwa kumuwekea miwa, wanapenda sana miwa.

“Kwa kawaida mkishabeba banda alimo na kuliingiza kwenye gari maalumu, ndipo mnamdunga sindano.

“Kwenye banda hilo alikuwa akiingia na kutoka kwa mwezi mmoja, ilipofika Desemba 8, 2015, ndipo akapelekwa eneo la Sasakwa, Grumeti,” alieleza mmoja wa wahifadhi aliyeshiriki kumhamisha faru huyo.

Mhifadhi huyo alilieleza gazeti hili kwamba kazi ya kumhamisha faru John ilifanywa na watu 56 na magari 15, na baada ya kumfikisha, timu ya madaktari ilibaki Sasakwa kwa siku saba kufuatilia maendeleo yake.

“Kule Sasakwa kwanza aliwekwa kwenye eneo dogo ili iwe rahisi kumfuatilia, lakini ilipofika Januari 8, mwaka huu, alifunguliwa na kuachwa kwenye eneo kubwa la wazi, na afya yake ilikuwa vizuri na alikuwa na mahusiano mazuri na faru jike aliyekuwa eneo hilo,” alieleza mhifadhi mwingine.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa faru John alianza kuonekana amezubaa tofauti na uchangamfu wa awali na ilipofika Agosti 20, mwaka huu, hali yake ilibadilika na kuwa mbaya kiasi cha kusimama kwa shida, jambo linalotajwa kuwashtua hata madaktari waliokuwa wakimwangalia.

Inadaiwa alipoteza maisha usiku wa kuamkia Agosti 21.

Mhifadhi huyo alisema kuwa faru John alikufa akiwa na umri wa miaka 38, miaka mitatu zaidi ya wastani wa maisha ya faru ambao ni miaka 35.

Alisema kuwa baada ya kifo chake uchunguzi wa kitaalamu kubaini sababu za kupoteza kwake maisha ulifanyika na kuhudhuriwa na madaktari kadhaa na wanafunzi zaidi ya 50 kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA).

Miongoni wa madaktari wanaotajwa kushiriki ni Dk. Morris Kilewo (TANAPA), Dk. Ernest Mjingo (TAWIRI), Dk. Emmanuel Macha (TANAPA), Dk. Justin Samanche (TAWIRI) na Profesa Donald Mpanduji wa SUA.

Taarifa nyingine zinasema kuwa baada ya uchunguzi huo, pembe mbili za faru John zilikabidhiwa kwa Mhifadhi wa Ikorongo-Grumeti, ambaye ni mtumishi wa wizara ili kuzipeleka Dar es Salaam ambako nyara za Serikali zinahifadhiwa katika jengo la Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii (Mpingo House).

Pia pembe kubwa ya faru John ilikuwa imewekwa kifaa maalumu cha utambuzi (transponder), ambacho hadi sasa kipo ndani ya pembe hiyo, na kinachotakiwa ni kuweka betri na kupata taarifa kuhusu faru huyo, njia ambayo inatajwa kuwa bora kuliko vipimo vya vinasaba (DNA).

Baadhi ya wahifadhi ambao wamehojiwa na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Serikali kuchunguza kile kinachotajwa kuwa “utata kifo cha Faru John”, walisema suala hilo lilipaswa kufanywa na wataalamu wa wanyamapori.

“Jamani hili suala ni la kitaalamu zaidi, sasa tulitarajia iundwe timu ya wataalamu waliobobea katika masuala ya wanyamapori ifanye kazi kwanza, kisha kama kutaonekana kuna kosa la jinai, sasa kikosi kazi kingeingia kazini kuchunguza,” alisema mmoja wa wahifadhi waliohojiwa.

Desemba 6, mwaka huu akiwa ziarani mkoani Arusha, Waziri Mkuu aliuagiza uongozi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, umletee nyaraka zote zilizotumika kumhamisha faru John kutoka hifadhi hiyo ifikapo Alhamisi, Desemba 8.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo alipotembelea ofisi za Makao Makuu ya NCAA zilizopo wilayani Ngorongoro, mkoani Arusha na kuzungumza na watumishi wa mamlaka hayo pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafugaji, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kikazi mkoani humo.

Saa 7 usiku Desemba 9, Waziri Mkuu alipokea taarifa inayoelezea utaratibu uliotumika kumhamisha faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko katika Hifadhi ya Grumeti.

Akizungumza katika kikao kilichofanyika nyumbani kwake Oysterbay, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Maghembe na baadhi ya watendaji wa wizara yake, Waziri Mkuu alisema taarifa hiyo itafanyiwa kazi na wataalamu wa ofisi yake.

Akisoma taarifa hiyo mbele ya Waziri Mkuu, Profesa Maghembe alisema hadi kufikia Desemba 2015 wakati faru John anahamishwa, alikuwa na watoto 26 (sawa na asilimia 70.2) ya faru wote waliokuwapo ndani ya kreta.

“Kati ya faru 37 waliokuwapo ndani ya kreta, watoto wake walikuwa 26 sawa na asilimia 70.2. Uamuzi wa kumwondoa John ulikuwa ni muhimu, ili kuwezesha kuongezeka kwa faru weusi na kupunguza tatizo la ‘inbreeding’ ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro.”

Baada ya kuhamishiwa Sasakwa, Waziri Maghembe alisema Julai 10, mwaka huu afya ya faru John ilianza kudorora na alikufa Agosti 18, mwaka huu. Taarifa hiyo iliandaliwa na Kamati ya Taifa ya Kuwalinda Tembo na Faru.

Akikabidhi pembe za faru huyo mbele ya Waziri Mkuu, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha Kupambana na Ujangili wa Wanyamapori, Robert Mande, alimweleza kwamba pembe kubwa ya faru John ilikuwa na uzito wa kilo 3.6 na ndogo ilikuwa na uzito wa kilo 2.3.

Mbali ya Waziri Mkuu kupokea ripoti na pembe za faru huyo, lakini siku tatu baada ya agizo hilo, maofisa watano wa NCAA wanaotuhumiwa kushiriki kumwondoa faru John kutoka katika kreta hiyo walikamatwa kwa mahojiano, ili kujua ukweli kuhusu mazingira ya kupotea kwake.

Pia Waziri Mkuu aliituhumu menejimenti na wafanyakazi wa NCAA kuwa imejaa vitendo vya rushwa na wizi na asingeweza kuvumilia sakata la faru John, ambaye alisema kuwa aliuzwa kwa Sh milioni 200 kwenye Hoteli ya Grumeti iliyo Hifadhi ya Serengeti na kuwa walipokea fedha za awali Sh milioni 100.

Waziri Mkuu alisema anataka kumwona faru huyo, nyaraka za kumhamisha na kama amekufa basi apelekewe hata pembe ofisini kwa kuwa anajua pa kuzipeleka.

Alisisitiza kuwa ikibainika kuna ambao wamekiuka taratibu watawajibika.

Hawa Ndio Wasanii 3 Ambao Lulu Anawakubali Kwenye Bongo Fleva

Msanii mahiri wa filamu Bongo, Elizabeth Michael aka Lulu amewataja wasanii watatu anaowakubali kwenye muziki wa Bongo Fleva.

Muigizaji huyo alikuwa akijibu swali la mmoja wa mashabiki wake kwenye mtandao wa Twitter, lililokuwa linauliza “wasanii gani watatu anaowakubali kwenye Bongo Fleva?”

Lulu alijibu swali hilo kwa kuandika, “Beka, Maua Sama na Alikiba.”

Watu 6 wanaswa na silaha kwa mganga wa kienyeji Mwanza

Taarifa Ya Jeshi La Polisi Mkoa Wa Mwanza Kwa Vyombo

Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 13:00hrs Katika Eneo La Buswelu Kata Ya Buswelu Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Wakiwa Katika Misako Na Doria Walifanikiwa Kuwakamata Watu Sita Wakiwa Na Silaha Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Pamoja Na Risasi Ishirini Na Tatu, Ambazo Walikuwa Wakizitumia Katika Matukio Ya Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Hapa Jijini Mwanza Na Mikoa Mingine.

Aidha Tukio Hilo Limefanikiwa Baada Ya Kupokea Taarifa Kutoka Kwa Raia Wema Kuhusu Uwepo Wa Wahalifu Hao, Ndipo Askari Walifanikiwa Kumkamata Kwanza Jeremiah Maligia @ Mkumbo Miaka 25, Mnyiramba, Fundi Seremala Mkazi Wa Malega – Singida Ambaye Alipohojiwa Alikiri Kuhusika Na Kutaja Wenzake Waliokuwa Wakishirikiana, Na Kuwa Silaha Wamezificha Kwa Mganga Wa Kienyeji Aitwaye Leornad Litta @ Makai Anayeishi Mtaa Wa Kagida – Buswelu.

Askari Walikwenda Mahali Hapo Na Kufanikiwa Kumkamata Mganga Huyo Wa Kienyeji Bwana Leornad Litta Miaka 39, Akiwa Na  Silaha Hizo Mbili Zilizotengenezwa Kienyeji Hapo Nyumbani Kwake Na Risasi Ishirini Na Mbili Zinazotumiwa Na Bunduki Ya Aina Ya Short Gun Na Risasi Moja Ya Rifle Aina Ya Mark Iv.

Aidha Katika Kuhojiwa Zaidi  Na Askari Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Waliwataja Washirika Wao Wanne Ambao Walikuwa Wakishirikiana Katika Kufanya Uhalifu Ambapo Askari Walifanikiwa Kuwakamata, Ambao Ni 1. Kamgisha Jovini Kamhambwa Miaka 40, Mlinzi Na Mkazi Wa Iloganzala, 2. Juma Yusuph @ Jimi Miaka 35, Mkazi Wa Bwani Kinondoni, 3. Samweli Peter Miaka 36, Mkazi Wa Busweli Na 4. Shabani Hussein Miaka 26, Fundi Viatu Na Mkazi Wa Nyasaka Msumbiji.

Watuhumiwa Wote Walipofanyiwa Mahojiano Walikiri Kwamba Silaha Hizo Walizitumia Katika Unyang’anyi Wa Mali Na Uporaji Katika Maeneo Ya Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Aidha Jeshi La Polisi Kwa Sasa Linaendelea Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo Na Matukio Waliyokuwa Wameyafanya, Pindi Uchunguzi Ukikamilika Watuhumiwa Wote Watafikishwa Mahakamani.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuendelea Na Tabia Ya Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi Lao La Polisi, Ili Tuweze Kudhibiti Uhalifu Katika Mkoa Wetu., Lakini Pia Anatoa Angalizo Kwa Wananchi Haswa Vijana Akiwataka Kuacha

Tabia Ya Kujihusisha Na Uhalifu Bali Wajikite Katika Kufanya Shughuli Halali Za Maendeleo, Kwani Jeshi La Polisi Lipo Vizuri

Kuhakikisha Ulinzi Na Usalama Upo Kwa Raia Wote Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza.

Katika Tukio La Pili

Mnamo Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 14:00hrs Mchana Katika Eneo La Ilemela Wilaya Ya Ilemela Jiji Na Mkoa Wa Mwanza, Askari Walifanikiwa Kuwakamata Watu Wawili Ambao Ni 1. Rahim Feka Miaka 28, Mkazi Wa Ilala – Dar Es Salaam, 2.  Ally Kawalale Miaka 32, Mkazi Wa Jetrumo – Arport Dar Es Salaam, Wakiwa Wanataka Kuuza Gari Lenye Namba T.778 Azv Aina Ya Toyota Land Cruiser Lililokuwa Wameliiba Huko Ilala Jijini Dar Es Salaam.

Aidha Watuhumiwa Hao Walikamatwa  Baada Ya Kupokelewa Taarifa Ya Kuibiwa Kwa Gari Hilo Huko Dar Es Salaam Na Kwamba Kuna Uwezekano Kuwepo Eneo La Kanda Ya Ziwa, Ndipo Ulifanyika Upelelzi Kuhusiana Na Taarifa Hiyo, Na Kufanikiwa Kuwakamata Watuhumiwa Tajwa Hapo Juu Wakiwa Na Gari Hilo.

Watuhumiwa Wote Wapo Chini Ya Ulinzi Wa Jeshi La Polisi Wakiendelea Na Mahojiano , Huku Taratibu Za Kuwasafirisha Kwenda Dar Es Salaam Wakiwa Chini Ya Ulinzi  Wa Askari Polisi Zikiwa Bado Zinaendelea.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Rai Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kuacha Tabia Ya Kununua Vitu Vya Wizi, Bali Pindi Wanapoona Biashara Za Wizi Zinataka Kufanyika Au Zinafanyika Watoe Taarifa Polisi Ili Watuhumiwa Waweze Kukamatwa Na Kufikishwa Mahakamani.

Katika Tukio La Tatu

Kwamba Tarehe 18.10.2016 Majira Ya Saa 23:00hrs Katika Kitongoji Cha Ibungiro Kijiji Cha Sagani Kata Ya Kandawe Wilaya Ya Magu Mkoa Wa Mwanza, Mtu Mmoja Msichana Aliyejulikana Kwa Jina La Dema Charles @ Bulayi Miaka 20, Mkazi Wa Kandawe, Ameuawa Kwa Kukatwa Na Vitu Vyenye Ncha Kali Sehemu Za Kichwani Na Kiunoni

Akiwa Amelalala Na Watu Wasiojulikana, Huku Wenzake Wa Wili Wakijeruhiwa Sehemu Mbalimbali Za Miili Yao.

Majeruhi Waliojeruhiwa Katika Tukio Hilo Ni 1.mariam Lucas @ Kapele Miaka 26, Mkazi Wa  Kijiji Cha Sagani Aliyejeruhiwa  Shingoni Na Kwenye Kiganja Cha Mkono Wa Kulia, 2. Kapelele Makubi @ Salulo Miaka 90, Ambaye Ni Baba Mwenye Nyumba/ Mji, Aliyejeruhiwa Mgongoni, Kichwani Na Kiunoni.

Inadaiwa Kuwa Wauaji Hao Walifika Katika Nyumba Hiyo Majira Tajwa Hapo Juu Na Kuwakuta Wenye Mji  Wakiwa Wamelala, Ndipo Waliingia Ndani Na Kufanya Mauaji Hayo, Hadi Sasa Hakuna Mtu Yeyote Aliyekamatwa Kuhusiana Na Tukio Hilo.

Aidha Uchunguzi Wa Awali Umebainisha Kuwa Mauji Hayo Yametokana Na Kulipiza Kisasi, Jeshi La Polisi Kwa Sasa Lipo Katika Upelezi Pamoja Na Uchunguzi Kuhusiana Na Tukio Hilo, Majeruhi Wapo Katika Hospitali Ya Wilaya Ya Magu Wakiendelea Kupatiwa Matibabu Na Hali Zao Zinaendelea Vizuri.

Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Mwanza Naibu Kamishina Wa Polisi Ahmed Msangi Anatoa Wito Kwa Wakazi Wa Jiji Na Mkoa Wa Mwanza Akiwataka Kutoa Ushirikiano Kwa Jeshi La Polisi Ili Watuhumiwa Wa Mauaji Hayo Wawezwe Kukamatwa Na Kufikishwa Katika Vyombo Vya Sheria.

Imetolewa Na:

Dcp: Ahmed Msangi

Kamanda Wa Polisi (M) Mwanza

Majambazi Hatari Wauawa.....Bunduki 9 Zakamatwa

Jeshi la polisi limedai kwamba limeua majambazi wawili  hatari na kukamata bunduki tisa, kati ya hizo SMG saba, shotgun moja na riffle moja, risasi 473 na magazini 16 baada ya majibizano ya risasi katika misitu ya Milima ya Usambara, Kijiji cha Magamba wilayani Lushoto. 
Katika majibizano hayo, pia polisi walidai kukamata bendera zenye maandishi ya lugha ya Kiarabu, redio saba za upepo na soksi za kuficha nyuso.
 
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Polisi, Nsato Marijani alisema jana kuwa hiyo ilikuwa operesheni ya kuwasaka majambazi waliovamia Chuo Kikuu cha Sekomu, wilayani humo hivi karibuni.
Alisema katika tukio hilo, askari wawili walijeruhiwa kwa risasi. Marijani ambaye alikuwa katika milima hiyo inayodaiwa kuwa ngome ya majambazi hao, aliwataja waliouawa kuwa ni Mudrick Abdi (24) maarufu kwa jina la Osama, mkazi wa Mbagala Majimatitu Dar es Salaam na Sultan Abdallah (24) mkazi wa Kiembesamaki, Zanzibar. 
Alisema askari waliojeruhiwa wanaendelea na matibabu na kwamba hawakupata madhara makubwa kwa kuwa walikuwa wamevaa majaketi ya kuzuia kupenya risasi .

Waziri Kairuki Afanya Ziara Dar, Kinondoni Kukagua Mradi Wa TASAF.......Asisitiza Waliotafuna Fedha Hizo Watatumbuliwa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki amesema atahakikisha anawachukulia hatua watendaji wote, walioshiriki katika udanganyifu wa kuingiza kaya zisizostahili katika Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

Aidha, aliiagiza Tasaf kuhakikisha inafuatilia kaya zote ambazo ziliingizwa katika mpango huo bila kuwa na sifa zinazostahili, kwa kuziorodhesha kwa majina, wanapoishi na kiasi cha fedha walichopokea ili ripoti hiyo iwasilishwe kwa Rais John Magufuli.

Kairuki aliyasema hayo jana wakati akizungumza baada ya kupokea ripoti ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (Tasaf III) ya Mkoa wa Dar es Salaam, sambamba na kuzungumza na wananchi katika mitaa ya Kigogo Kati na Mikoroshoni, Manispaa ya Kinondoni.

“Kaya ambazo hazistahili hawafanyi peke yao wanashirikiana na watu, kama ni viongozi katika ngazi za mitaa na kata mitaa tunataka majina, na katika kila jina tujue nani alishiriki kumuingiza nani alikuwa akimchukulia na kama yupo mtumishi wetu wa umma tujue ni nani na hatua gani za kinidhamu zimechukuliwa.”
 “...Msije mkashangaa nikaja kuelekeza polisi kukamata hawa na hawa kwa sababu hizi hela ni lazima zirudi,” alisema Kairuki.

Alisema ameshapokea taarifa za mikoa mbalimbali, lakini Dar es Salaam na wilaya zake bado na mwisho ilikuwa ni Oktoba 6, mwaka huu, lakini aliwaongeza wiki moja ambayo tayari imeisha na orodha hiyo inatakiwa ipelekwe kwa Rais Magufuli.

Kairuki aliongeza kuwa pamoja na mkoa kusema umeondoa kaya 789 ambazo hazina sifa, lakini kuna kaya 5,457 ambazo zinapaswa kuondolewa katika mpango huo kwa kuwa hazina sifa za kupokea ruzuku hiyo. 
“...baada ya kuelekeza uhakiki wa nyumba kwa nyumba, sisi kwa taarifa tulizonazo tutaondoa kaya 5,457. Sasa ujiulize nyinyi ndio mlikuwa katika zoezi na mkapata idadi hiyo, hapa inaonesha kuna kitu hakipo sawa,” alisema.

Alisema katika kaya hizo zitakazoondolewa, 1,867 hazina vigezo vya umasikini, 563 zipo kwenye orodha lakini zilikuwa hazijitokezi kuchukua ruzuku na hazijulikani zilipo na kaya nyingine 2,114 hazikupatikana wala kujulikana zilipo wakati wa ukaguzi.

Alisema kaya hizi ni nyingi na hasa ikizingatiwa asilimia 76 hazijaingizwa katika mpango huo, hivyo kaya hizo ambazo ziliandikishwa zinapaswa kwenda kukaguliwa ili ziweze kuingizwa katika mpango huo ili katika awamu ya nane ya uhawilishaji fedha waweze kupata.

Kairuki alisema kiasi kikubwa cha fedha kimepotea, ambacho kingeweza kuwasaidia watu wanaostahili kuwa katika mpango huo. 
Alisema wilaya za Kinondoni na Temeke zimeshapokea malipo ya awamu saba ambayo ni Sh bilioni 6.7. Alisema hadi sasa kuna kaya 32,456 zilizoondolewa kwenye mpango huo.

Kwa wastani kaya moja hulipwa kati ya Sh 20,000 hadi 60,000 kwa kutegemea idadi ya watu katika kaya.

Akizungumza katika mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ali Hapi ambaye pia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa alisema mpango huo ni muhimu kwa maendeleo ya taifa, lakini kuna watu wanaoharibu taswira ya Tasaf.

Alisema kuna fedha nyingi ambazo zinaishia kwenye mikono ya wajanja na haziwafikii walengwa wa mpango huo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tasaf, Ladislaus Mwamanga alisema mpango huo umeandaliwa kitaalamu na utaendelea kuwa endelevu na kwamba mradi huo unategemea zaidi serikali na wafadhili, lakini hadi sasa kiasi kikubwa kimekuwa kikitoka kwa wafadhili.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa umma na Utawala bora Mh. Angela Kairukia akiwa sambamba na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,akiendelea na ziara katika Mkoa wa Dar es salaam kukagua maendeleo ya mradi wa kusaidia kaya masikini TASAF

Nyota ya Godbless Lema Inavyomng'arisha RC Gambo Mbele ya Rais Magufuli

Kama mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema anapambana na Mrisho Gambo ili kujijenga kwa wananchi wake, basi mkuu huyo wa mkoa ananufaika na vita hiyo na anatarajia makubwa zaidi baada ya mzozo wa mwanzoni mwa wiki.

Wakati Gambo akitarajia kupandishwa cheo na Rais John Magufuli, madiwani wa jiji hilo wametangaza kususia vikao vyote hadi viongozi wa juu wa Serikali watakapoingilia kati mgogoro uliopo.

Wawili hao waliingia kwenye mzozo mwingine mapema wiki hii wakati Gambo alipoalikwa kuzindua ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto, itakayojengwa kwa ufad kwa ufadhili wa taasisi ya Martenity Africa alipojaribu kueleza historia ya kiwanja cha jengo hilo, maelezo ambayo Lema aliyapinga kwa sauti kubwa na kusababisha shughuli hiyo kuvurugika.

Baada ya mzozo huo, Gambo amedokeza kuwa kuna makubwa yanafuata.

“Baada ya hilo, simu zilikuja kibao, lakini bahati nzuri kabla sijauliza kokote, na Mheshimiwa Rais ndio akawa ananipigia akaniambia nina full confidence (nina imani) na wewe. Labda wafikirie promotion (kupandisha cheo), lakini hayo mengine hayapo,” alisema Gambo akiwaeleza wafanyabiashara wa mjini hapa kuhusu barua iliyosambaa juzi kwenye mitandao ya kijamii kuwa Rais ametengua uteuzi wake.

“Baadaye (Rais) akaniambia kwamba sasa ili (wafanyabiashara) wajue kwamba kweli nimekupigia simu, niitie mmoja uliye naye karibu ili niongee naye. Ndio (mwenyekiti wa wafanyabiashara wa Arusha) akapata previledge (bahati) naye ya kuongea na Mheshimiwa Rais.”

Iwapo Gambo atapandishwa cheo, ambacho kwa mukhtadha wa utumishi wa umma chaweza kuwa ni kuteuliwa kuwa mbunge na baadaye waziri, itakuwa ni mara ya pili kupanda cheo siku chache baada ya kuzozana na Lema.

Gambo, ambaye aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha Juni 26, alilumbana na Lema Agosti Mosi mbele na Naibu Waziri wa Tamisemi, Suleiman Jafo.

Katika tukio hilo, Lema alisema Gambo haheshimu mipaka ya kazi zake, akimtuhumu kuingilia maamuzi ambayo tayari yameshajadiliwa kwenye vikao halali vya halmashauri na kupitishwa na ofisi ya mkuu wa mkoa katika kikao cha wakuu wa idara, maofisa tarafa, waratibu wa elimu kata watumishi wa Mamlaka ya Maji Safi na Mazingira (Auwsa) jijini hapa.

“Nimeona nizungumze hapahapa ili naibu waziri ufahamu hali ilivyo hapa. Kwa mfano Baraza la Madiwani la mwaka 2008, ndilo lililopitisha kiwango cha posho kwa madiwani kutoka Sh100,000 hadi 120,000. Jambo la kushangaza DC ameandika barua Tamisemi na nakala kwa Takukuru ili wachunguze jambo ambalo limeshapata baraka za Tamisemi,” alisema Lema.

Hali hiyo ilimfanya naibu waziri kuingilia kati na kuahidi kuzishughulikia changamoto hizo na kumpa nafasi Gambo, ambaye wakati huo alikuwa mkuu wa wilaya, kujibu hoja hizo. 
“Mheshimiwa mbunge nataka ujue mimi ndiyo mkuu wa shughuli za Serikali hapa wilayani. Muda wowote nina uwezo wa kuingilia kati mambo ambayo naona hayaendi sawa, hata kama yupo katibu tawala na viongozi wengine,” alisema Gambo.

“Rais aliona ninafaa ndiyo maana akaniteua na sihitaji kujifunza namna ya kuwa mkuu wa wilaya  kwa kuwa huu ni mwaka tano.”

Malumbano hayo yaliendelea na kumuhusisha pia Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye aliungana na Lema na madiwani wengine kupinga jambo hilo.

Baada ya vuta nikuvute hiyo mbele ya waziri, Agosti 18 Gambo aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuchukua nafasi ya Felix Ntibenda.

Siku chache baada ya uteuzi huo, Gambo aliagiza halmashauri ya jiji kutafuta fedha za kupunguza deni la walimu ambalo ni Sh154 milioni. 
Mkurugenzi wa jiji hilo, Athuman Kilamia alitangaza posho za madiwani ambazo zilikuwa zinalipwa kinyume cha taratibu, zitumike kupunguza deni la walimu na zikatolewa.

Mgogoro ukaibuka kati ya madiwani wa jiji hilo ambao wengi ni kutoka Chadema.

Sakata la Jumanne wiki hii linaweza kumpa cheo kikubwa zaidi kutokana na Rais Magufuli kumpigia simu kwa lengo la kumthibitishia kuwa yuko pamoja naye siku ambayo barua ya kughushi ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mkuu huyo wa nchi ametengua uteuzi wa Gambo.

Sakata hilo lilitokea katika uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto jijini Arusha ambao utagharimu Sh9 bilioni, sehemu kubwa ya fedha hizo zikitoka taasisi ya Martenity Africa.

Mvutano huo ulianza baada ya Gambo kusema kuwa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa hospitali imetolewa na Taasisi ya Mawalla Fund kwa kuwa muasisi wake, Nyaga Mawalla alikuwa na maono ya kusaidia afya ya mama na mtoto.

Kauli yake ilikuwa ikimaanisha kuwa Mfuko wa Maendeleo wa Arusha (ArDF) haikutoa kiwanja hicho kwa Martenity Africa wala kutafuta mfadhili.

Jambo hilo liliwakera viongozi wa ArDF, ambayo imeanzishwa na Lema na Elifuraha Mlowe, ambaye ni mwenyekiti. 
Lema alimtaka ndugu wa wakili huyo amsahihishe Gambo, lakini hakuna kilichofanyika, ndipo aliposimama na kuanza kupinga kwa sauti maelezo ya Gambo.

Lema alikuwa akisema mkuu huyo wa mkoa anapotosha ukweli kwa misingi ya kisiasa, kwa kuwa Mawalla Fund ilitoa kiwanja hicho kwa ArDF, ambayo ilitafuta wafadhili na kusaini nao mkataba wa ujenzi wa hospitali.

Wageni kwenye hafla hiyo iliyofanyika Bulka walijaribu kuwatuliza wawili hao, hawakufanikiwa kutokana na Lema kuendelea kueleza kwa sauti kuwa Gambo anapotosha, huku mkuu huyo wa mkoa akizungumza kwenye kipaza sauti kumtaka mbunge huyo atulie.

Shughuli hiyo ilimalizika kiutata na hivyo waandaaji wakashindwa kuendesha harambee iliyopangwa kufanyika baada ya uzinduzi.

Juma Nature: Kuna Watu Wanahonga Ili Ngoma Zangu Zisipigwe

Ukizungungumzia historia ya muziki wa Bongo Flava, haiwezi kukamilika bila kulitaja jina la mkongwe Juma Kassim Nature aliyewahi kutamba ngoma kama ‘Jinsi Kijana’, ‘Hili Game’ na zingine kibao.

Hatimaye mkongwe huyo amaibuka na kudai kuwa kuna watu wanahonga ili nyimbo zake na za TMK Halisi zisichezwe redioni.

Nature amesema kuwa miongoni mwa watu hao ni uongozi wake wa zamani lakini hakuwa tayari kuwataja kwa majina.

“Sasa hivi kuna urasimu, kuna watu wanaenda kuhonga nyimbo zangu zisipigwe za Halisi zisipigwe, wapo watu wanafanya issue kama hizo na tayari tumeshaingia in deep kujua nini tatizo kwanini nyimbo hazichezwi,” ameniambia Nature nilipozungungumza naye nyumbani kwake Temeke.

Ikumbukwe Nature alikuwa akifanya kazi chini ya kundi la Wanaume Family kundi linalomilikiwa na Said Fella kabla ya kujitoa kwenye kundi na baadhi ya wasanii wengine waliokuwa kwenye kundi hilo na kuanzisha kundi lao jipya linalofahamika kama Wanaume Halisi.

Serikali Yakubali Kurejesha Posho ya Sh. 8500 kwa Siku kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Nchini

Bodi ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetuliza hasira za wanafunzi wa vyuo vikuu kwa kurejesha posho ya chakula na malazi ya Sh8,500 kwa kila mmoja na kwamba tofauti baina yao itakuwa viwango vya ada.

Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku kama ilivyokuwa awali. 
 
Hatua ya wanafunzi kujenga umoja ili kushinikiza haki katika posho ilitokana na baadhi yao kuingiziwa kati ya Sh40,000 na 70,000 badala ya Sh 510,000, hali ambayo ilizua sintofahamu. 
Ndalichako alisema tofauti ya malipo itakuwa katika ada na siyo posho, “Vigezo vya mikopo vimebadilika, kila mwanafunzi atapata fedha tofauti lakini tumefanya marekebisho kwenye posho ya chakula ambayo kila mwanafunzi atalipwa Sh8,500 kama awali.” 
Kwa mujibu wa utaratibu wa Bodi hiyo, malipo hayo ya chakula na malazi hutolewa kila baada ya miezi miwili. 

Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo. 
Rais wa Daruso, Erasmi Leon alisema hayo jana wakati akizungumza na wanafunzi wenzake kuhusu kusudio la kwenda HESLB kwa ajili ya kutafuta haki yao ya msingi. 
“Ninachowasihi tuwe pamoja. Tuwe wamoja na twende pamoja. Tutakwenda wawakilishi kutafuta nafasi kwa amani waweze kusikia tuna hoja gani lakini tukinyimwa hii nafasi tutaenda kuitafuta tukiwa wengi,” alisema na kuongeza:
 “Tuwe watulivu kwa sasa tutakapowahitaji muda na wakati wowote kwa lolote tushirikiane ili twende pamoja tumalize pamoja tuhakikishe tunapata Sh8,500 kwa kila mwanafunzi kwa chakula na malazi,” alisema. 
Kuhusu suala hilo, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ulisema wajibu wake ni kupokea na kusambaza majina na taarifa kutoka Bodi kwa wanafunzi. 
Akitoa ufafanuzi kwa wanafunzi waliofika ofisini kwake kujua hatima yao na waliopata mikopo kuchukua fomu za kutia saini, Ofisa Mikopo wa UDSM, Lugano Mwakyusa alisema wenye jukumu la kujua walio na sifa ya kupata mikopo ni Bodi ya Mikopo. 
“Tunaendelea kupokea majina kutoka bodi. Tayari hapa kuna majina 949 yameshatoka, wengine tuzidi kusubiri na wale mwaka wa pili na tatu ambao walikuwa na mitihani ya marudio taarifa zao zitapelekwa bodi,” Mwakyusa aliwaambia wanafunzi waliokuwa wamejaa ofisini kwake.
 Kulikuwa na hali ya sintofahamu chuoni hapo jana baada ya wanafunzi wengi wa mwaka wa kwanza kuonekana wakiwa wameshika bahasha za kaki zilizokuwa na fomu za usajili wanazotakiwa kujaza huku wakihangaika kutokana na kutojua kiasi cha mkopo. 
Juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, AbdulRazaq Badru alieleza kwamba ingawa wanafunzi 88,000 waliomba mikopo kutoka HESLB, uwezo wa bodi hiyo ni kutoa kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa na asilimia 24 na waliokuwa wameshapatiwa walikuwa 11,000 sawa na asilimia 12. 
Takwimu hizi zinaonyesha zaidi ya robo tatu ya wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.

Feza Kessy Anahisi Nando Anadata ‘Atafutwe na Asaidiwe’

Staa aliyewahi kuiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother Africa, Feza Kessy, amesema kuwa anaamini Nando aliyewahi kushiriki naye kwenye shindano hilo, amepatwa na tatizo au anaugua kwakuwa tabia anazozionyesha zinampa mashaka.

Akiongea kwenye kipindi cha Kubamba kupitia Times FM, Feza amesema anaona akili ya Nando kama imevurugika kwa sasa. Anasema amekuwa tofauti na Nando, yule kijana mwenye nidhamu na mpole aliyekuwa akimfahamu.

“Naamini Nando ana tatizo asaidiwe,” alisema Feza. “Sijui kwanini lakini naamini Nando ana something hayupo sawa, sio yule Nando ninayemfahamu, naomba atafutwe asaidiwe,” alisisitiza.

Feza ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa Choice FM, amedai kuwa aliwahi kukutana na Nando na akampa noti ya shilingi elfu 10. Anasema badala yake yake staa huyo aliitupa chini kwa madai kuwa haiwezi kumsaidia kitu.

Wema Sepetu a.k.a Tanzania Sweatheart Kuolewa Hivi Karibuni

Kwa taarifa nilizozinyaka hivi karibuni hukooo Instagram ni kuwa kipenzi cha wengi ( najua wengi mtabisha) si mwingine mrembo wetu Miss TZ 2006 na CEO wa kampuni ya ENDLESS FAME the one & only WEMA ABRAHAM ISAC SEPETU anaolewa hivi karibuni na model anaekuja kwa spidi ya 4G CALISAH ABDULHAMID.

Though hawaja comfirm wenyewe kuhusiana na habari hii ila nimejiongeza tu mwenyewe baada ya kuzinyaka picha hizi...